Magonjwa ya kuku

Chicken vaccine

Ni kawaida hadi asilimia 1 ya vifaranga wako kufa ndani ya wiki ya kwanza. Zaidi ya hiyo, unaweza kuwa na tatizo, kama ugonjwa. Magonjwa kama Ugonjwa wa kideri ama sotoka na Gumboro hayana tiba. Kuku wako wote wanaweza kufa kwa haraka sana. Chanja kuku wako kuzuia magonjwa.




Dalili za Ugonjwa wa Sokota sokota(Newcastle Disease/NCD)

Newcastle Disease symptoms

Chanja kwa ajili ya NCD(Kideri) siku ya 7 na 21. Weka tone moja la chanjo kwenye jicho la kuku au tundu ya pua. Ngoja kuku apepese au avute pumzi ndani. Nunua chanjo kutoka kwa wauza pembejeo. Chanjo inaitwa Avivax Kenya na Temevac Tanzania. Chupa 1 inachanja kuku 50. Chanja kila miezi 3.


Dalili za Gumboro

Peleka aliekufa kuku kwa dakitari wa mifugo achune ngozi. Kama kuna alama za damu, kuku wako amekufa kutokana na Gumboro.

Gumboro blood stains

Chanja Gumboro siku ya 10 na siku ya 14.

Changanya chanjo pamoja na maji ya kunywa ya kuku. Usiwape kuku maji kwa saa 1 – hadi 2 kabla ya chanjo. Watakua na kiu na hivyo watakunywa chanjo.