Kujenga banda la Ng’ombe

Cow Shed

Hii ni sehemu kwaajili ya ng’ombe kupumzika na kulala wakati wa usiku. Kila ng’ombe ana nafasi yake katika eneo la kumpuzikia, linaitwa . Vyuma lazima vifunikwe na paa lilotengezwa kwa mabati, nyasi au makuti.

Paa lazima liwe juu vya kutosha ili lisiliwe na ng’ombe kama limetengenezwa kwa nyasi au hay inahifadhiwa chini yake.

Vyumba lazima vijengwe kiasi kwamba ng’ombe anabakia msafi muda wote.

Safisha banda la ng’ombe kila siku.

Sakafu ya zege itamzuia ng’ombe asiteleze. Sakafu yenye mwinuko itasaidia uchafu kutoka na ujikusanye nje ya banda.

Safisha na weka viuatilifu kwenye sakafu kila siku. Hii inazuia kuoza kwa kwako na nyayo.

Ng’ombe anahitaji nafasi ya kulala. Mtu anapaswa kujenga idadi ya kutosha ya vyumba ili kutosheleza ng’ombe muda wote. Vyumba visivyotumika ni uharibifu wa nafasi na pesa.

Cow shed interior

Kwa idadi ya ng’ombe kwa kila vyumba, vyumba vya ziada vinahitajika kuweza kuweka ndama wadogo ( mitamba) na kadhalika.

  • Ng’ombe 1 vyumba 2
  • Ng’ombe 2 vyumba 3
  • Ng’ombe 3 vyumba 5
  • Ngombe 4 vyumba 6
  • Ng’ombe 5 vyumba 7
  • Ng’ombe 6 vyumba 9

Chumba kina urefu wa 210cm ( futi 7) na upana wa 120 cm ( futi 4). Vyumba vinatenganishwa na mbao 2. Ng’ombe hawatakiwi kuzunguka ndani ya chumba.

Chakula ndani ya sehemu ya kulia angalau futi 3 juu ya ardhi. Weka jiwe la madini katika kila chumba kuzuia kupigana kati ya wanyama.