Nini kinatokea usipolipa mkopo wako?

Loans pay on time

Kuna vitu vingi vinaweza kutokea wakati usipoheshimu mkataba wa marejesho yako ya mkopo:

  • Utalipishwa ada au riba ya ziada na kuongezewa kwenye mkopo wako.
  • Unaweza kushtakiwa kwa Mamlaka ya Dhamana ya Mkopo( Credit Reference Bureau)
  • Mkopeshaji wako anaweza kuwaambia wakusanyaji wa madeni kujaribu na kupata unachodaiwa kutoka kwako.Kwenye hili wakulima wengi wameripoti mifugo na hata mashamba yao kuchukuliwa na benki na wakopeshaji wengine.
  • Unaweza kushtakiwa mahakamani ambapo unalazimishwa kulipa mkopo wako au kutumikia kifungo jela.
  • Unahatarisha kupoteza dhamana yako.
  • Kama ulikua na wadhamini wa mkopo, wanaweza kulazimishwa kulipa mkopo huo kwa niaba yako.
  • Unaweza kuwa na wakati mgumu kupata mkopo mwingine huko mbeleni/sikuzijazo